Mfumo wa Majitaka

Kwa sasa mamlaka haina mfumo wa uondoaji majitaka na kupelekea huduma ya uondoaji majitaka kufanywa na Manispaa ya Shinyanga kupitia idara ya afya.

Katika mpango wa maendeleo wa sekta ya maji (WSDP) awamu ya kwanza mtalaam muelekezi ambaye ni GIBB Afrika amekamilisha kazi ya kuandaa makablasha ya miundombinu hiyo na kuwasilisha wizara ya maji kwa hatua zaidi.

Matarajio yaliyopo ni kwamba, katika utekelezaji wa mpango wa maendeleo wa sekta ya maji awamu ya pili (WSDP II) na kama fedha itapatikana ujenzi wa mfumo wa uondoaji majitaka unaweza kutekelezwa.



Tovuti Zinazohusiana

NEMC
KASHWASA
Bonde la Ziwa Viktoria
Tovuti ya Taifa

Kupata Namba za Malipo

Kupata ankara yako na huduma nyingine, tafadhali fuata hatua zifuatazo;

  1. Piga *152*00#
  2. Chagua 6; Maji
  3. Chagua 1; Huduma za Maji za Pamoja
  4. Chagua Huduma Unayoitaka
  5. Ingiza Namba ya Akaunti (A476... au B476...)
Njia za Kufanya Malipo