Historia Yetu
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga ilianzishwa rasmi tarehe 1/7/1998 kwa mujibu wa Sheria ya Maji (Cap 281) kifungu cha 3(1) ya mwaka 1997 iliyofanyiwa marekebisho na Sheria Na.12 ya Maji na Usafi wa Mazingira ya mwaka 2009
Sheria hiyo imezipa Mamlaka za Maji na Usafi wa Mazingira nchini majukumu ya kuendesha shughuli zote za maji chini ya uongozi wa Bodi ya Wakurugenzi walioteuliwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji kutokana na mapendekezo ya uongozi wa Mkoa. Bodi hiyo ina wajumbe 10 wanaowakilisha makundi mbalimbali ya jamii.