Usambazaji Maji

Usambazaji wa Mitandao

Mamlaka imegawanya eneo lake la huduma katika kanda nne; Kanda ya Kati, Kanda ya Kaskazini, kanda ya Kusini na Kanda ya Mashariki. Matandao wa mabomba una urefu wa km 548.24 yanayounganisha kanda zote nne. Mfumo mpya (Maji kutoka ziwa viktoria) una urefu wa km338.74 wenye mabomba ya uPVC na chuma ya kuanzia kipenyo cha mm110, Maji hupelekwa kwenye matanki manne yaliyo kwenye miinuko ndani ya Manispaa ya Shinyanga kwa urefu wa km27 yenye vipenyo kati ya mm400 hadi mm900. Matanki yamewekwa kwenye miiniuko kwa lengo la kupata mgandamizo wa maji unaotakiwa kusambaza maji katika Manispaa yote. Matanki haya yana mitaza ujazo 250 kila moja yenye uwezo wa kusambaza maji kama ifuatavyo:-

  
Na. Kanda Urefu wa mtandao (km)
1 Kanda ya Kati 140.47
2 Kanda ya kusini 137.48
3 Kanda ya Kasikazini 68.94
4 Kanda ya Mashariki 16.90
5 Mfumo wa zamani 184.45
Jumla 548.24
    

Tovuti Zinazohusiana

NEMC
KASHWASA
Bonde la Ziwa Viktoria
Tovuti ya Taifa

Kupata Namba za Malipo

Kupata ankara yako na huduma nyingine, tafadhali fuata hatua zifuatazo;

  1. Piga *152*00#
  2. Chagua 6; Maji
  3. Chagua 1; Huduma za Maji za Pamoja
  4. Chagua Huduma Unayoitaka
  5. Ingiza Namba ya Akaunti (A476... au B476...)
Njia za Kufanya Malipo